Zab. 143:7-11 Swahili Union Version (SUV)

7. Ee BWANA, unijibu hima, roho yangu imelegea;Usinifiche uso wako,Nisifanane nao washukao shimoni

8. Unifanye kusikia fadhili zako asubuhi,Kwa maana nimekutumaini Wewe.Unijulishe njia nitakayoiendea,Kwa maana nakuinulia nafsi yangu.

9. Ee BWANA, uniponye na adui zangu;Nimekukimbilia Wewe, unifiche.

10. Unifundishe kuyatenda mapenzi yako,Kwa maana ndiwe Mungu wangu;Roho yako mwema aniongoze kwenye nchi sawa,

11. Ee BWANA, unihuishe kwa ajili ya jina lako,Kwa haki yako unitoe roho yangu taabuni;

Zab. 143