5. Nimezikumbuka siku za kale,Nimeyatafakari matendo yako yote,Naziwaza kazi za mikono yako.
6. Nakunyoshea mikono yangu;Nafsi yangu inakuonea kiu kama nchi kame.
7. Ee BWANA, unijibu hima, roho yangu imelegea;Usinifiche uso wako,Nisifanane nao washukao shimoni
8. Unifanye kusikia fadhili zako asubuhi,Kwa maana nimekutumaini Wewe.Unijulishe njia nitakayoiendea,Kwa maana nakuinulia nafsi yangu.
9. Ee BWANA, uniponye na adui zangu;Nimekukimbilia Wewe, unifiche.