4. Na roho yangu imezimia ndani yangu,Moyo wangu ndani yangu umesituka.
5. Nimezikumbuka siku za kale,Nimeyatafakari matendo yako yote,Naziwaza kazi za mikono yako.
6. Nakunyoshea mikono yangu;Nafsi yangu inakuonea kiu kama nchi kame.
7. Ee BWANA, unijibu hima, roho yangu imelegea;Usinifiche uso wako,Nisifanane nao washukao shimoni
8. Unifanye kusikia fadhili zako asubuhi,Kwa maana nimekutumaini Wewe.Unijulishe njia nitakayoiendea,Kwa maana nakuinulia nafsi yangu.
9. Ee BWANA, uniponye na adui zangu;Nimekukimbilia Wewe, unifiche.
10. Unifundishe kuyatenda mapenzi yako,Kwa maana ndiwe Mungu wangu;Roho yako mwema aniongoze kwenye nchi sawa,
11. Ee BWANA, unihuishe kwa ajili ya jina lako,Kwa haki yako unitoe roho yangu taabuni;