Zab. 140:3-7 Swahili Union Version (SUV)

3. Wamenoa ndimi zao kama nyoka,Sumu ya fira i chini ya midomo yao.

4. Ee BWANA, unilinde na mikono ya mtu asiye haki;Unihifadhi na mtu wa jeuri;Waliowaza kuzipotosha hatua zangu.

5. Wenye kiburi wamenifichia mtego na kamba;Wametandika wavu kando ya njia;Wameniwekea matanzi.

6. Nimemwambia BWANA, Ndiwe Mungu wangu;Ee BWANA, uisikie sauti ya dua zangu.

7. Ee MUNGU Bwana, nguvu za wokovu wangu,Umenifunika kichwa changu siku ya vita.

Zab. 140