Zab. 140:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Ee BWANA, uniokoe na mtu mbaya,Unihifadhi na mtu wa jeuri.

2. Waliowaza mabaya mioyoni mwao,Kila siku huondokesha vita.

3. Wamenoa ndimi zao kama nyoka,Sumu ya fira i chini ya midomo yao.

4. Ee BWANA, unilinde na mikono ya mtu asiye haki;Unihifadhi na mtu wa jeuri;Waliowaza kuzipotosha hatua zangu.

5. Wenye kiburi wamenifichia mtego na kamba;Wametandika wavu kando ya njia;Wameniwekea matanzi.

Zab. 140