Zab. 136:12-25 Swahili Union Version (SUV)

12. Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

13. Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

14. Akawavusha Israeli katikati yake;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

15. Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

16. Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

17. Yeye aliyewapiga wafalme wakuu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

18. Akawaua wafalme mashuhuri;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

19. Sihoni, mfalme wa Waamori;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

20. Na Ogu, mfalme wa Bashani;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

21. Akaitoa nchi yao iwe urithi;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

22. Urithi wa Israeli mtumishi wake;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

23. Aliyetukumbuka katika unyonge wetu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

24. Akatuokoa na watesi wetu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

25. Kila chenye mwili akipa chakula chake;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

Zab. 136