Zab. 136:1-8 Swahili Union Version (SUV)

1. Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

2. Mshukuruni Mungu wa miungu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

3. Mshukuruni Bwana wa mabwana;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

4. Yeye peke yake afanya maajabu makuu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

5. Yeye aliyefanya mbingu kwa fahamu zake;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

6. Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

7. Yeye aliyefanya mianga mikubwa;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

8. Jua litawale mchana;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

Zab. 136