Zab. 136:1-16 Swahili Union Version (SUV)

1. Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

2. Mshukuruni Mungu wa miungu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

3. Mshukuruni Bwana wa mabwana;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

4. Yeye peke yake afanya maajabu makuu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

5. Yeye aliyefanya mbingu kwa fahamu zake;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

6. Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

7. Yeye aliyefanya mianga mikubwa;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

8. Jua litawale mchana;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

9. Mwezi na nyota zitawale usiku;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

10. Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wa kwanza wao;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

11. Akawatoa Waisraeli katikati yao;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

12. Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

13. Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

14. Akawavusha Israeli katikati yake;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

15. Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

16. Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani;Kwa maana fadhili zake ni za milele.

Zab. 136