Zab. 135:6-14 Swahili Union Version (SUV)

6. BWANA amefanya kila lililompendeza,Katika mbingu na katika nchi,Katika bahari na katika vilindi vyote.

7. Ndiye apandishaye mvuke toka miisho ya nchi;Huifanyia mvua umeme;Hutoa upepo katika hazina zake.

8. Aliwapiga wazaliwa wa kwanza wa Misri,Wa wanadamu na wa wanyama.

9. Alipeleka ishara na maajabu kati yako, Ee Misri,Juu ya Farao na watumishi wake wote.

10. Aliwapiga mataifa mengi,Akawaua wafalme wenye nguvu;

11. Sihoni, mfalme wa Waamori,Na Ogu, mfalme wa Bashani,Na falme zote za Kanaani.

12. Akaitoa nchi yao iwe urithi,Urithi wa Israeli watu wake.

13. Ee BWANA, jina lako ni la milele,BWANA, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.

14. Kwa kuwa BWANA atawaamua watu wake,Atawahurumia watumishi wake.

Zab. 135