Zab. 119:44-48 Swahili Union Version (SUV)

44. Nami nitaitii sheria yako daima,Naam, milele na milele.

45. Nami nitakwenda panapo nafasi,Kwa kuwa nimejifunza mausia yako.

46. Nitazinena shuhuda zako mbele ya wafalme,Wala sitaona aibu.

47. Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako,Ambayo nimeyapenda.

48. Na mikono yangu nitayainulia maagizo yako niliyoyapenda,Nami nitazitafakari amri zako.

Zab. 119