Zab. 119:43-45 Swahili Union Version (SUV)

43. Usiliondoe neno la kweli kinywani mwangu kamwe,Maana nimezingojea hukumu zako.

44. Nami nitaitii sheria yako daima,Naam, milele na milele.

45. Nami nitakwenda panapo nafasi,Kwa kuwa nimejifunza mausia yako.

Zab. 119