Zab. 119:42-54 Swahili Union Version (SUV)

42. Nami nitamjibu neno anilaumuye,Kwa maana nalitumainia neno lako.

43. Usiliondoe neno la kweli kinywani mwangu kamwe,Maana nimezingojea hukumu zako.

44. Nami nitaitii sheria yako daima,Naam, milele na milele.

45. Nami nitakwenda panapo nafasi,Kwa kuwa nimejifunza mausia yako.

46. Nitazinena shuhuda zako mbele ya wafalme,Wala sitaona aibu.

47. Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako,Ambayo nimeyapenda.

48. Na mikono yangu nitayainulia maagizo yako niliyoyapenda,Nami nitazitafakari amri zako.

49. Likumbuke neno ulilomwambia mtumishi wako,Kwa sababu umenitumainisha.

50. Hii ndiyo faraja yangu katika taabu yangu,Ya kwamba ahadi yako imenihuisha.

51. Wenye kiburi wamenidharau mno,Sikujiepusha na sheria zako.

52. Nimezikumbuka hukumu zako za kale,Ee BWANA, nikajifariji.

53. Ghadhabu imenishika kwa sababu ya wasio haki,Waiachao sheria yako.

54. Amri zako zimekuwa nyimbo zangu,Katika nyumba ya ugeni wangu.

Zab. 119