40. Tazama, nimeyatamani mausia yako,Unihuishe kwa haki yako.
41. Ee BWANA, fadhili zako zinifikie na mimi,Naam, wokovu wako sawasawa na ahadi yako.
42. Nami nitamjibu neno anilaumuye,Kwa maana nalitumainia neno lako.
43. Usiliondoe neno la kweli kinywani mwangu kamwe,Maana nimezingojea hukumu zako.