Zab. 119:170-175 Swahili Union Version (SUV)

170. Dua yangu na ifike mbele zako,Uniponye sawasawa na ahadi yako.

171. Midomo yangu na itoe sifa,Kwa kuwa unanifundisha mausia yako.

172. Ulimi wangu na uiimbe ahadi yako,Maana maagizo yako yote ni ya haki.

173. Mkono wako na uwe tayari kunisaidia,Maana nimeyachagua mausia yako.

174. Ee BWANA, nimeutamani wokovu wako,Na sheria yako ndiyo furaha yangu.

175. Nafsi yangu na iishi, ipate kukusifu,Na hukumu zako zinisaidie.

Zab. 119