146. Nimekuita Wewe, uniokoe,Nami nitazishika shuhuda zako.
147. Kutangulia mapambazuko naliomba msaada,Naliyangojea maneno yako kwa tumaini.
148. Macho yangu yalitangulia makesha ya usiku,Ili kuitafakari ahadi yako.
149. Uisikie sauti yangu sawasawa na fadhili zako,Ee BWANA, unihuishe sawasawa na hukumu yako.
150. Wanakaribia wanaonifuatia kwa chuki,Wamekwenda mbali na sheria yako.
151. Ee BWANA, Wewe U karibu,Na maagizo yako yote ni kweli.
152. Tokea zamani nimejua kwa shuhuda zako,Ya kuwa umeziweka zikae milele.
153. Uyaangalie mateso yangu, uniokoe,Maana sikuisahau sheria yako.
154. Unitetee na kunikomboa,Unihuishe sawasawa na ahadi yako.
155. Wokovu u mbali na wasio haki,Kwa maana hawajifunzi amri zako.
156. Ee BWANA, rehema zako ni nyingi,Unihuishe sawasawa na hukumu zako.
157. Wanaonifuatia na watesi wangu ni wengi,Lakini sikujiepusha na shuhuda zako.
158. Nimewaona watendao uhaini nikachukizwa,Kwa sababu hawakulitii neno lako.