Zab. 119:139-143 Swahili Union Version (SUV)

139. Juhudi yangu imeniangamiza,Maana watesi wangu wameyasahau maneno yako.

140. Neno lako limesafika sana,Kwa hiyo mtumishi wako amelipenda.

141. Mimi ni mdogo, nadharauliwa,Lakini siyasahau mausia yako.

142. Haki yako ni haki ya milele,Na sheria yako ni kweli.

143. Taabu na dhiki zimenipata,Maagizo yako ni furaha yangu.

Zab. 119