Zab. 119:130-134 Swahili Union Version (SUV)

130. Kufafanusha maneno yako kwatia nuru,Na kumfahamisha mjinga.

131. Nalifunua kinywa changu nikatweta,Maana naliyatamani maagizo yako.

132. Unigeukie, unirehemu mimi,Kama iwahusuvyo walipendao jina lako.

133. Uzielekeze hatua zangu kwa neno lako,Uovu usije ukanimiliki.

134. Unikomboe na dhuluma ya mwanadamu,Nipate kuyashika mausia yako.

Zab. 119