Zab. 119:126-130 Swahili Union Version (SUV)

126. Wakati umewadia BWANA atende kazi;Kwa kuwa wameitangua sheria yako.

127. Ndiyo maana nimeyapenda maagizo yako,Kuliko dhahabu, naam, dhahabu iliyo safi.

128. Maana nayaona mausia yako yote kuwa ya adili,Kila njia ya uongo naichukia.

129. Shuhuda zako ni za ajabu,Ndiyo maana roho yangu imezishika.

130. Kufafanusha maneno yako kwatia nuru,Na kumfahamisha mjinga.

Zab. 119