Zab. 119:119-123 Swahili Union Version (SUV)

119. Wabaya wa nchi pia umewaondoa kama takataka,Ndiyo maana nimezipenda shuhuda zako.

120. Mwili wangu unatetemeka kwa kukucha Wewe,Nami ninaziogopa hukumu zako.

121. Nimefanya hukumu na haki,Usiniache mikononi mwao wanaonionea.

122. Uwe mdhamini wa mtumishi wako, apate mema,Wenye kiburi wasinionee.

123. Macho yangu yamefifia kwa kuutamani wokovu wako,Na ahadi ya haki yako.

Zab. 119