Zab. 119:116-123 Swahili Union Version (SUV)

116. Unitegemeze sawasawa na ahadi yako, nikaishi,Wala usiniache niyaaibikie matumaini yangu.

117. Unisaidie nami nitakuwa salama,Nami nitaziangalia amri zako daima.

118. Umewakataa wote wazikosao amri zako,Kwa maana hila zao ni uongo.

119. Wabaya wa nchi pia umewaondoa kama takataka,Ndiyo maana nimezipenda shuhuda zako.

120. Mwili wangu unatetemeka kwa kukucha Wewe,Nami ninaziogopa hukumu zako.

121. Nimefanya hukumu na haki,Usiniache mikononi mwao wanaonionea.

122. Uwe mdhamini wa mtumishi wako, apate mema,Wenye kiburi wasinionee.

123. Macho yangu yamefifia kwa kuutamani wokovu wako,Na ahadi ya haki yako.

Zab. 119