101. Nimeiepusha miguu yangu na kila njia mbaya,Ili nilitii neno lako.
102. Sikujiepusha na hukumu zako,Maana Wewe mwenyewe umenifundisha.
103. Mausia yako ni matamu sana kwangu,Kupita asali kinywani mwangu.
104. Kwa mausia yako najipatia ufahamu,Ndiyo maana naichukia kila njia ya uongo.
105. Neno lako ni taa ya miguu yangu,Na mwanga wa njia yangu.
106. Nimeapa nami nitaifikiliza,Kuzishika hukumu za haki yako.
107. Nimeteswa mno;Ee BWANA, unihuishe sawasawa na neno lako.
108. Ee BWANA, uziridhie sadaka za kinywa changu,Na kunifundisha hukumu zako.
109. Nafsi yangu imo mkononi mwangu daima,Lakini sheria yako sikuisahau.
110. Watendao uovu wamenitegea mtego,Lakini sikuikosa njia ya mausia yako.
111. Shuhuda zako nimezifanya urithi wa milele,Maana ndizo changamko la moyo wangu.
112. Nimeuelekeza moyo wangu nizitende amri zako,Daima, naam, hata milele.
113. Watu wa kusita-sita nawachukia,Lakini sheria yako naipenda.