Zab. 118:8-14 Swahili Union Version (SUV)

8. Ni heri kumkimbilia BWANAKuliko kuwatumainia wanadamu.

9. Ni heri kumkimbilia BWANA.Kuliko kuwatumainia wakuu.

10. Mataifa yote walinizunguka;Kwa jina la BWANA naliwakatilia mbali.

11. Walinizunguka, naam, walinizunguka;Kwa jina la BWANA naliwakatilia mbali.

12. Walinizunguka kama nyuki,Walizimika kama moto wa miibani;Kwa jina la BWANA naliwakatilia mbali.

13. Ulinisukuma sana ili nianguke;Lakini BWANA akanisaidia.

14. BWANA ni nguvu zangu na wimbo wangu,Naye amekuwa wokovu wangu.

Zab. 118