Zab. 118:23-28 Swahili Union Version (SUV)

23. Neno hili limetoka kwa BWANA,Nalo ni ajabu machoni petu.

24. Siku hii ndiyo aliyoifanya BWANA,Tutashangilia na kuifurahia.

25. Ee BWANA, utuokoe, twakusihi;Ee BWANA, utufanikishe, twakusihi.

26. Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la BWANA;Tumewabarikia toka nyumbani mwa BWANA.

27. BWANA ndiye aliye Mungu,Naye ndiye aliyetupa nuru.Ifungeni dhabihu kwa kambaPembeni mwa madhabahu.

28. Ndiwe Mungu wangu, nami nitakushukuru,Ndiwe Mungu wangu, nami nitakutukuza.

Zab. 118