Zab. 118:10-16 Swahili Union Version (SUV)

10. Mataifa yote walinizunguka;Kwa jina la BWANA naliwakatilia mbali.

11. Walinizunguka, naam, walinizunguka;Kwa jina la BWANA naliwakatilia mbali.

12. Walinizunguka kama nyuki,Walizimika kama moto wa miibani;Kwa jina la BWANA naliwakatilia mbali.

13. Ulinisukuma sana ili nianguke;Lakini BWANA akanisaidia.

14. BWANA ni nguvu zangu na wimbo wangu,Naye amekuwa wokovu wangu.

15. Sauti ya furaha na wokovuImo hemani mwao wenye haki;Mkono wa kuume wa BWANA hutenda makuu.

16. Mkono wa kuume wa BWANA umetukuzwa;Mkono wa kuume wa BWANA hutenda makuu.

Zab. 118