Zab. 116:2-7 Swahili Union Version (SUV)

2. Kwa maana amenitegea sikio lake,Kwa hiyo nitamwita siku zangu zote.

3. Kamba za mauti zilinizunguka,Shida za kuzimu zilinipata.Naliona taabu na huzuni;

4. Nikaliitia jina la BWANA.Ee BWANA, nakuomba sana,Uniokoe nafsi yangu.

5. BWANA ni mwenye neema na haki,Naam, Mungu wetu ni mwenye rehema.

6. BWANA huwalinda wasio na hila;Nalidhilika, akaniokoa.

7. Ee nafsi yangu, urudi rahani mwako,Kwa kuwa BWANA amekutendea ukarimu.

Zab. 116