Zab. 11:4-6 Swahili Union Version (SUV)

4. BWANA yu katika hekalu lake takatifu.BWANA ambaye kiti chake kiko mbinguni,Macho yake yanaangalia;Kope zake zinawajaribu wanadamu.

5. BWANA humjaribu mwenye haki;Bali nafsi yake humchukia asiye haki,Na mwenye kupenda udhalimu.

6. Awanyeshee wasio haki mitego,Moto na kiberiti na upepo wa hari,Na viwe fungu la kikombe chao.

Zab. 11