2. Na waseme hivi waliokombolewa na BWANA,Wale aliowakomboa na mkono wa mtesi.
3. Akawakusanya kutoka nchi zote,Mashariki na magharibi, kaskazini na kusini.
4. Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika;Hawakuona mji wa kukaa.
5. Waliona njaa, waliona na kiu,Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao.
6. Wakamlilia BWANA katika dhiki zao,Akawaponya na shida zao.
7. Akawaongoza kwa njia ya kunyoka,Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa.