13. Wakamlilia BWANA katika dhiki zao,Akawaponya na shida zao.
14. Aliwatoa katika giza na uvuli wa mauti,Akayavunja mafungo yao.
15. Na wamshukuru BWANA kwa fadhili zake,Na maajabu yake kwa wanadamu.
16. Maana ameivunja milango ya shaba,Ameyakata mapingo ya chuma.
17. Wapumbavu, kwa sababu ya ukosaji wao,Na kwa sababu ya maovu yao, hujitesa.
18. Nafsi zao zachukia kila namna ya chakula,Wameyakaribia malango ya mauti.
19. Wakamlilia BWANA katika dhiki zao,Akawaponya na shida zao.
20. Hulituma neno lake, huwaponya,Huwatoa katika maangamizo yao.
21. Na wamshukuru BWANA kwa fadhili zake,Na maajabu yake kwa wanadamu.