Zab. 107:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema,Kwa maana fadhili zake ni za milele.

2. Na waseme hivi waliokombolewa na BWANA,Wale aliowakomboa na mkono wa mtesi.

3. Akawakusanya kutoka nchi zote,Mashariki na magharibi, kaskazini na kusini.

Zab. 107