Zab. 106:43-47 Swahili Union Version (SUV)

43. Mara nyingi aliwaponya,Bali walikuwa wakimwasi kwa mashauri yao,Wakadhilika katika uovu wao.

44. Lakini aliyaangalia mateso yao,Aliposikia kilio chao.

45. Akawakumbukia agano lake;Akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake;

46. Akawajalia kuhurumiwaNa watu wote waliowateka.

47. Ee BWANA, Mungu wetu, utuokoe,Utukusanye kwa kututoa katika mataifa,Tulishukuru jina lako takatifu,Tuzifanyie shangwe sifa zako.

Zab. 106