43. Mara nyingi aliwaponya,Bali walikuwa wakimwasi kwa mashauri yao,Wakadhilika katika uovu wao.
44. Lakini aliyaangalia mateso yao,Aliposikia kilio chao.
45. Akawakumbukia agano lake;Akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake;
46. Akawajalia kuhurumiwaNa watu wote waliowateka.
47. Ee BWANA, Mungu wetu, utuokoe,Utukusanye kwa kututoa katika mataifa,Tulishukuru jina lako takatifu,Tuzifanyie shangwe sifa zako.