Zab. 106:24-28 Swahili Union Version (SUV)

24. Wakaidharau nchi ile ya kupendeza,Wala hawakuliamini neno lake.

25. Bali wakanung’unika hemani mwao,Wala hawakuisikiliza sauti ya BWANA.

26. Ndipo alipowainulia mkono wake,Ya kuwa atawaangamiza jangwani,

27. Na kuwatawanya wazao wao kati ya mataifa,Na kuwatapanya katika nchi mbali.

28. Wakajiambatiza na Baal-Peori,Wakazila dhabihu za wafu.

Zab. 106