Zab. 106:15-30 Swahili Union Version (SUV)

15. Akawapa walichomtaka,Akawakondesha roho zao.

16. Wakamhusudu Musa matuoni,Na Haruni, mtakatifu wa BWANA.

17. Nchi ikapasuka ikammeza Dathani,Ikaufunika mkutano wa Abiramu.

18. Moto ukawaka katika mkutano wao,Miali yake ikawateketeza wabaya.

19. Walifanya ndama huko Horebu,Wakaisujudia sanamu ya kuyeyuka.

20. Wakaubadili utukufu waoKuwa mfano wa ng’ombe mla majani.

21. Wakamsahau Mungu, mwokozi wao,Aliyetenda makuu katika Misri.

22. Matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu,Mambo ya kutisha penye bahari ya Shamu.

23. Akasema ya kuwa atawaangamizaKama Musa, mteule wake, asingalisimama,Mbele zake kama mahali palipobomoka,Ili aigeuze hasira yake asije akawaharibu.

24. Wakaidharau nchi ile ya kupendeza,Wala hawakuliamini neno lake.

25. Bali wakanung’unika hemani mwao,Wala hawakuisikiliza sauti ya BWANA.

26. Ndipo alipowainulia mkono wake,Ya kuwa atawaangamiza jangwani,

27. Na kuwatawanya wazao wao kati ya mataifa,Na kuwatapanya katika nchi mbali.

28. Wakajiambatiza na Baal-Peori,Wakazila dhabihu za wafu.

29. Wakamkasirisha kwa matendo yao;Tauni ikawashambulia.

30. Ndipo Finehasi akasimama akafanya hukumu;Tauni ikazuiliwa.

Zab. 106