Zab. 105:23-27 Swahili Union Version (SUV)

23. Israeli naye akaingia Misri,Yakobo akawa mgeni katika nchi ya Hamu.

24. Akawajalia watu wake wazae sana,Akawafanya kuwa hodari kuliko watesi wao.

25. Akawageuza moyo wawachukie watu wake,Wakawatendea hila watumishi wake.

26. Akamtuma Musa, mtumishi wake,Na Haruni ambaye amemchagua.

27. Akaweka mambo ya ishara zake kati yao,Na miujiza katika nchi ya Hamu.

Zab. 105