10. Alilomthibitishia Yakobo liwe amri,Na Israeli liwe agano la milele.
11. Akisema, Nitakupa wewe nchi ya Kanaani,Iwe urithi wenu mliopimiwa.
12. Walipokuwa watu wawezao kuhesabiwa,Naam, watu wachache na wageni ndani yake,
13. Wakatanga-tanga toka taifa hata taifa,Toka ufalme mmoja hata kwa watu wengine.
14. Hakumwacha mtu awaonee,Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao.
15. Akisema, Msiwaguse masihi wangu,Wala msiwadhuru nabii zangu.
16. Akaiita njaa iijilie nchi,Akakiharibu chakula chote walichokitegemea.
17. Alimpeleka mtu mbele yao,Yusufu aliuzwa utumwani.
18. Walimwumiza miguu yake kwa pingu,Akatiwa katika minyororo ya chuma.
19. Hata wakati wa kuwadia neno lake,Ahadi ya BWANA ilimjaribu.
20. Mfalme alituma watu akamfungua,Mkuu wa watu akamwachia.
21. Akamweka kuwa bwana wa nyumba yake,Na mwenye amri juu ya mali zake zote.
22. Awafunge masheki wake kama apendavyo,Na kuwafundisha wazee wake hekima.
23. Israeli naye akaingia Misri,Yakobo akawa mgeni katika nchi ya Hamu.
24. Akawajalia watu wake wazae sana,Akawafanya kuwa hodari kuliko watesi wao.
25. Akawageuza moyo wawachukie watu wake,Wakawatendea hila watumishi wake.
26. Akamtuma Musa, mtumishi wake,Na Haruni ambaye amemchagua.
27. Akaweka mambo ya ishara zake kati yao,Na miujiza katika nchi ya Hamu.
28. Alituma giza, kukafunga giza,Wala hawakuyaasi maneno yake.