Zab. 104:8-15 Swahili Union Version (SUV)

8. Yakapanda milima, yakatelemka mabondeni,Mpaka mahali ulipoyatengenezea.

9. Umeweka mpaka yasiupite,Wala yasirudi kuifunikiza nchi.

10. Hupeleka chemchemi katika mabonde;Zapita kati ya milima;

11. Zamnywesha kila mnyama wa kondeni;Punda mwitu huzima kiu yao.

12. Kandokando hukaa ndege wa angani;Kati ya matawi hutoa sauti zao.

13. Huinywesha milima toka orofa zake;Nchi imeshiba mazao ya kazi zako.

14. Huyameesha majani kwa makundi,Na maboga kwa matumizi ya mwanadamu;Ili atoe chakula katika nchi,

15. Na divai imfurahishe mtu moyo wake.Aung’aze uso wake kwa mafuta,Na mkate umburudishe mtu moyo wake.

Zab. 104