7. Kwa kukemea kwako yakakimbia,Kwa sauti ya radi yako yakaenda zake kasi,
8. Yakapanda milima, yakatelemka mabondeni,Mpaka mahali ulipoyatengenezea.
9. Umeweka mpaka yasiupite,Wala yasirudi kuifunikiza nchi.
10. Hupeleka chemchemi katika mabonde;Zapita kati ya milima;
11. Zamnywesha kila mnyama wa kondeni;Punda mwitu huzima kiu yao.