Zab. 104:7-11 Swahili Union Version (SUV)

7. Kwa kukemea kwako yakakimbia,Kwa sauti ya radi yako yakaenda zake kasi,

8. Yakapanda milima, yakatelemka mabondeni,Mpaka mahali ulipoyatengenezea.

9. Umeweka mpaka yasiupite,Wala yasirudi kuifunikiza nchi.

10. Hupeleka chemchemi katika mabonde;Zapita kati ya milima;

11. Zamnywesha kila mnyama wa kondeni;Punda mwitu huzima kiu yao.

Zab. 104