Zab. 104:30-34 Swahili Union Version (SUV)

30. Waipeleka roho yako, wanaumbwa,Nawe waufanya upya uso wa nchi.

31. Utukufu wa BWANA na udumu milele;BWANA na ayafurahie matendo yake.

32. Aitazama nchi, inatetemeka;Aigusa milima, inatoka moshi.

33. Nitamwimbia BWANA maadamu ninaishi;Nitamshangilia Mungu wangu nikiwa hai;

34. Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake;Mimi nitamfurahia BWANA.

Zab. 104