Zab. 104:26-34 Swahili Union Version (SUV)

26. Ndimo zipitamo merikebu,Ndimo alimo lewiathani uliyemwumba acheze humo.

27. Hao wote wanakungoja Wewe,Uwape chakula chao kwa wakati wake.

28. Wewe huwapa,Wao wanakiokota;Wewe waukunjua mkono wako,Wao wanashiba mema;

29. Wewe wauficha uso wako,Wao wanafadhaika;Waiondoa pumzi yao, wanakufa,Na kuyarudia mavumbi yao,

30. Waipeleka roho yako, wanaumbwa,Nawe waufanya upya uso wa nchi.

31. Utukufu wa BWANA na udumu milele;BWANA na ayafurahie matendo yake.

32. Aitazama nchi, inatetemeka;Aigusa milima, inatoka moshi.

33. Nitamwimbia BWANA maadamu ninaishi;Nitamshangilia Mungu wangu nikiwa hai;

34. Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake;Mimi nitamfurahia BWANA.

Zab. 104