Zab. 104:13-17 Swahili Union Version (SUV)

13. Huinywesha milima toka orofa zake;Nchi imeshiba mazao ya kazi zako.

14. Huyameesha majani kwa makundi,Na maboga kwa matumizi ya mwanadamu;Ili atoe chakula katika nchi,

15. Na divai imfurahishe mtu moyo wake.Aung’aze uso wake kwa mafuta,Na mkate umburudishe mtu moyo wake.

16. Miti ya BWANA nayo imeshiba,Mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.

17. Ndimo ndege wafanyamo vitundu vyao,Na korongo, misunobari ni nyumba yake.

Zab. 104