Zab. 102:17-20 Swahili Union Version (SUV)

17. Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa,Asiyadharau maombi yao.

18. Kizazi kitakachokuja kitaandikiwa hayo,Na watu watakaoumbwa watamsifu BWANA.

19. Maana ametazama toka patakatifu pake pa juu,Toka mbinguni BWANA ameiangalia nchi,

20. Ili akusikie kuugua kwake aliyefungwa,Na kuwafungua walioandikiwa kufa.

Zab. 102