1. Ee BWANA, usikie kuomba kwangu,Kilio changu kikufikie.
2. Usinifiche uso wako siku ya shida yangu,Unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi.
3. Maana siku zangu zinatoweka kama moshi,Na mifupa yangu inateketea kama kinga.
4. Moyo wangu umepigwa kama majani na kukauka,Naam, ninasahau kula chakula changu.