1. Ee BWANA, kwa nini wasimama mbali?Kwani kujificha nyakati za shida?
2. Kwa kiburi chake asiye haki mnyonge anafuatiwa kwa ukali;Na wanaswe kwa hila zizo hizo walizoziwaza.
3. Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake,Na mwenye choyo humkana BWANA na kumdharau.
4. Mdhalimu kwa kiburi cha uso wakeAsema, Hatapatiliza.Jumla ya mawazo yake ni, Hakuna Mungu;