Yos. 21:38-40 Swahili Union Version (SUV)

38. Tena katika kabila ya Gadi Ramothi katika Gileadi pamoja na malisho yake, huo mji wa makimbilio kwa ajili ya mwuaji, na Mahanaimu pamoja na malisho yake;

39. na Heshboni pamoja na malisho yake, na Yazeri pamoja na malisho yake; jumla yake miji minne.

40. Miji hiyo yote ilikuwa ni miji ya wana wa Merari kwa kuandama jamaa zao, ni hizo jamaa za Walawi zilizosalia; na kura yao ilikuwa ni miji kumi na miwili.

Yos. 21