Yos. 21:19-24 Swahili Union Version (SUV)

19. Miji yote ya wana wa Haruni, makuhani, ilikuwa ni miji kumi na mitatu, pamoja na malisho yake.

20. Na jamaa za wana wa Kohathi, Walawi, hao wana wengine wa Kohathi waliosalia, wao walikuwa na miji ya kura yao katika kabila ya Efraimu.

21. Nao wakawapa Shekemu pamoja na malisho yake, katika nchi ya vilima ya Efraimu, huo mji wa makimbilio kwa ajili ya mwuaji; na Gezeri pamoja na malisho yake;

22. na Kibisaumu pamoja na malisho yake, na Beth-horoni pamoja na malisho yake, miji minne.

23. Tena katika kabila ya Dani Elteke pamoja na malisho yake, na Gibethoni pamoja na malisho yake;

24. na Aiyaloni pamoja na malisho yake, na Gath-rimoni pamoja na malisho yake; miji minne.

Yos. 21