14. na Yatiri pamoja na malisho yake, na Eshtemoa pamoja na malisho yake;
15. na Holoni pamoja na malisho yake, na Debiri pamoja na malisho yake;
16. na Aini pamoja na malisho yake, na Yuta pamoja na malisho yake, na Bethshemeshi pamoja na malisho yake; miji kenda katika kabila hizo mbili.
17. Tena katika kabila ya Benyamini, Gibeoni pamoja na malisho yake, na Geba pamoja na malisho yake;
18. na Anathothi pamoja na malisho yake, na Almoni pamoja na malisho yake; miji minne.
19. Miji yote ya wana wa Haruni, makuhani, ilikuwa ni miji kumi na mitatu, pamoja na malisho yake.