Yos. 18:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Kisha mkutano mzima wa wana wa Israeli walikutana pamoja hapo Shilo, wakasimamisha hema ya kukutania kuko; nayo nchi ilikuwa imeshindwa mbele zao.

2. Zilisalia katika wana wa Israeli kabila saba ambazo hazijagawanyiwa bado urithi wao.

3. Yoshua akawauliza wana wa Israeli, akasema, Je! Hata lini mtakuwa walegevu katika kuingia kwenu na kuimiliki hiyo nchi, ambayo yeye BWANA, Mungu wa baba zenu, amewapa?

Yos. 18