6. Musa mtumishi wa BWANA na wana wa Israeli wakawapiga; naye Musa mtumishi wa BWANA akawapa Wareubeni, na Wagadi, na nusu ya kabila ya Manase iwe urithi wao.
7. Hawa ni wafalme wa hiyo nchi ambao Yoshua na wana wa Israeli waliwapiga ng’ambo ya pili ya Yordani upande wa magharibi, kutoka Baal-gadi katika bonde la Lebanoni mpaka kilima cha Halaki, kilichoelekea Seiri; Yoshua naye akawapa kabila za Israeli iwe milki yao sawasawa na magawanyo yao;
8. katika nchi ya vilima, na katika Shefela, na katika nchi ya Araba, na katika matelemko, na katika bara, na katika Negebu; nchi ya Mhiti, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi;
9. mfalme wa Yeriko, mmoja; mfalme wa Ai, ulio karibu na Betheli, mmoja;
10. mfalme wa Yerusalemu, mmoja; mfalme wa Hebroni, mmoja;
11. mfalme wa Yarmuthi, mmoja; na mfalme wa Lakishi, mmoja;
12. mfalme wa Egloni, mmoja; na mfalme wa Gezeri, mmoja;
13. mfalme wa Debiri, mmoja; na mfalme wa Gederi, mmoja;
14. mfalme wa Horma, mmoja; na mfalme wa Aradi, mmoja;
15. mfalme wa Libna, mmoja; na mfalme wa Adulamu, mmoja;
16. mfalme wa Makeda, mmoja; na mfalme wa Betheli, mmoja;
17. mfalme wa Tapua, mmoja; na mfalme wa Heferi, mmoja;
18. mfalme wa Afeka, mmoja; na mfalme wa Lasharoni, mmoja;
19. mfalme wa Madoni, mmoja; na mfalme wa Hazori, mmoja;
20. mfalme wa Shimron-meroni, mmoja; na mfalme wa Akshafu, mmoja;