Yon. 2:7-10 Swahili Union Version (SUV)

7. Roho yangu ilipozimia ndani yangu,Nalimkumbuka BWANA;Maombi yangu yakakuwasilia,Katika hekalu lako takatifu.

8. Watu waangaliao mambo ya ubatili na uongoHujitenga na rehema zao wenyewe;

9. Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani;Nitaziondoa nadhiri zangu.Wokovu hutoka kwa BWANA.

10. BWANA akasema na yule samaki, naye akamtapika Yona pwani.

Yon. 2