Yon. 2:5-10 Swahili Union Version (SUV)

5. Maji yalinizunguka, hata nafsini mwangu;Vilindi vilinizunguka;Mwani ulikizinga kichwa changu;

6. Nalishuka hata pande za chini za milima;Hiyo nchi na mapingo yake yalinifunga hata milele;Lakini umeipandisha nafsi yangu kutoka shimoni,Ee BWANA, Mungu wangu,

7. Roho yangu ilipozimia ndani yangu,Nalimkumbuka BWANA;Maombi yangu yakakuwasilia,Katika hekalu lako takatifu.

8. Watu waangaliao mambo ya ubatili na uongoHujitenga na rehema zao wenyewe;

9. Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani;Nitaziondoa nadhiri zangu.Wokovu hutoka kwa BWANA.

10. BWANA akasema na yule samaki, naye akamtapika Yona pwani.

Yon. 2