5. Maji yalinizunguka, hata nafsini mwangu;Vilindi vilinizunguka;Mwani ulikizinga kichwa changu;
6. Nalishuka hata pande za chini za milima;Hiyo nchi na mapingo yake yalinifunga hata milele;Lakini umeipandisha nafsi yangu kutoka shimoni,Ee BWANA, Mungu wangu,
7. Roho yangu ilipozimia ndani yangu,Nalimkumbuka BWANA;Maombi yangu yakakuwasilia,Katika hekalu lako takatifu.
8. Watu waangaliao mambo ya ubatili na uongoHujitenga na rehema zao wenyewe;
9. Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani;Nitaziondoa nadhiri zangu.Wokovu hutoka kwa BWANA.
10. BWANA akasema na yule samaki, naye akamtapika Yona pwani.