Yoe. 2:11-16 Swahili Union Version (SUV)

11. naye BWANA anatoa sauti yake mbele ya jeshi lake; maana matuo yake ni makubwa sana; kwa maana yeye ni hodari atekelezaye neno lake; kwa kuwa siku ya BWANA ni kuu, yenye kitisho sana; naye ni nani awezaye kuistahimili?

12. Lakini hata sasa, asema BWANA, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea;

13. rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya.

14. N’nani ajuaye kwamba hatarudi na kugeuka, na kutuachia baraka nyuma yake, naam, sadaka ya unga, na sadaka ya kinywaji, kwa BWANA, Mungu wenu?

15. Pigeni tarumbeta katika Sayuni,Takaseni saumu, kusanyeni kusanyiko kuu;

16. Kusanyeni watu, litakaseni kusanyiko,Kusanyeni wazee, kusanyeni watoto,Na hao wanyonyao maziwa;Bwana arusi na atoke chumbani mwake,Na bibi arusi katika hema yake.

Yoe. 2